http://s3-us-west-2.amazonaws.com/millard-ayo-bucket/wp-content/uploads/2017/09/12124853/Kubenea.jpg

Thursday, March 21, 2013

YANGA YAENDELEA KUJIFUA


 
Kikosi cha timu ya Young Africans leo kimeendelea na mazoezi asubuhi katika uwanja wa mabatini Kijitonyama kujiandaa na mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi ya Vodacom dhidi ya timu ya Polisi Morogoro siku ya jumamosi  Machi 30 ,2013 katika dimba la Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Young Africans ambayo inaongoza msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa kuwa na pointi 48 na mabao 37 ya kufunga na mabao 12 ya kufunga, iko mbele kwa pointi 11 zaidi ya timu ya Azam inayoshika nafasi ya pili kwa kuwa na ponti 37 na mabao 32 ya kufunga na mabao 16 ya kufungwa.

Mara baada ya kupata ushindi wa tano mfululizo katika michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom, kikosi cha mholanzi Ernie Brandts kiliendelea na mazoezi katika uwanja wa mabatini Kijitonyama siku ya leo ikiwa ni sehemu ya maandalzi ya mchezo wa siku ya jumamosi.

Katika mchezo wa mwisho Young Africans iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya  Ruvu Shooting bao lililofungwa na mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Hamis Kiiza, tangu mzunguko wa pili uanze Yanga imeshacheza jumla ya michezo saba na kufanikiwa kushinda michezo sita na kutoka sare mmoja hivyo kujikusanyia pointi 19 kati ya 21.

Ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa Ubingwa, Kocha Mkuu Brandts amesema anakianadaa kikosi chake kuhakikisha kinapata pointi 3 katika kila mchezo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa Ubingwa.

"Kila mchezo tunaocheza kwa sasa ni fainali kwetu, kila timu inahitaji kupata pointi ili kujiweka katika nafasi nzuri, na sisi pia tunahitaji  kupata pointi 3 katika kila mchezo hali inayopelekea mechi kuwa ngumu, lakini kikubwa nimekiandaa kikosi changu kuhakikisha kinaibuka na pointi 3 katika kila mchezo" alisema Brandts
 
Katika mazoezi yaliyoanza tangu  jana wachezaji wote wanaendelea kujifua, ambapo wataendelea na mazoezi mpaka watakapoungana na wachezaji wenzao walioko katika timu za Taifa mbalimbali.
 
Yanga imetoa jumla ya wachezaji nane kwa ajili ya kuzitumikiia timu za taifa, wachezaji hao ni Klevin Yondano, Frank Domayo, Saimon Msuva, Nadir Haroub 'Cannavaro', na Athuman Idd 'Chuji'(Tanzania), Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite (Rwanda) na Hamis Kiiza (Uganda).
 
wachezaji wanaondelea na mazoezi ni :
 
Said Mohamed, Yusuph Abdul na Ally Mustafa 'Barthez' (magolikipa)
 
Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Salum Telela, Oscar Joshua, Godfrey Taita na Juma Abdul (walinzi)
 
Nurdin Bakari, Omega Seme na David Luhende, Reheni Kibingu (viungo) 
 
Jerson Tegete, Didier Kavumbagu na Said Bahanuzi 
 
Ladislaus Mbogo, George Banda na Nizar Khalfani ni wagonjwa hawakuweza kufanya mazoezi leo

No comments:

Post a Comment