 
Huwezi
 amini: Akitokea benchi, Demba Ba aliteleza na kupiga mpira uliozama 
kimiani na kuiandikia Chelsea bao la pili na la ushindi.
 
Mwanaume: Demba Ba akishangilia bao lake lililoipeleka Chelsea nusu fainali
 
Anafunga
 safari: Jose Mourinho akikimbia kuelekea eneo la kibendera cha kona 
baada ya Chelsea kufunga bao la pili na la muhimu mno usiku huu
 
Maelekezo: Mourinho akiwaambia wachezaji wake walinde bao hilo la ushindi katika dakika za majeruhi
MSENEGAL
 `Supa Sabu` Demba Ba ameibua shangwe, nderemo na vifijo kwa mashabiki 
wa Chelsea waliofurika katika dimba la Stamford Bridge usiku huu baada 
ya kuifungia klabu yake bao muhimu katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya 
PSG.
Hii
 ilikuwa mechi ya robo fainali ya pili ambayo Chelsea walihitaji ushindi
 wa mabao mawili kwa bila ili kufuzu hatua ya nusu fainali kufuatia 
kufungwa mabao 3-1 katika mchezo wa kwanza nchini Ufaransa.
Chelsea
 wamefuzu kwa faida ya bao la ugenini baada ya wastani wa magoli kuwa 
3-3, lakini kwa vile wao walifunga bao moja katika kipigo cha 3-1 nchini
 Ufaransa wameweza kufuzu hatua ya nusu fainali.
Ba
 alifunga bao la pili katika dakika ya 87 na kumfanya Kocha wa Chelsea 
Jose Mourinho ashangilie kama alivyofanya miaka ya nyuma akiwa na FC 
Porto.
Cesar
 Azpilicueta alipiga shuti ambalo liliwababatiza mabeki wa PSG na mpira 
kumkuta Ba akiwa eneo zuri na kumalizia kwa ufundi mkubwa mno huku 
mlinda mlango,Salvatore Sirigu akibaki hana la kufanya. 
Wakati
 kila mtu akiamini Mourinho ameshatupwa nje ya mashindano, ghafla baada 
ya bao la nyota huyo raia wa Senegal, Jose alikimbia kutoka eneo la 
benchi lake kwenda kwenye kibendera cha kona kushangilia na wachezaji 
wake.
Mourinho
 amewakumbusha watu wengi miaka ya nyuma kwani aliwahi kushangilia kwa 
staili hiyo akiwa na FC Porto mwaka 2004 kwenye uwanja wa Old Trafford.
Hakika usiku huu ni wa furaha kubwa kwa Mourinho 
kwasababu
 kadri muda ulivyozidi kwenda alikuwa anachanganyikiwa na kuona ndoto 
zake zinafifia mpaka ilipofika dakika hizo za lala salama na Ba 
kumnyanyua kwa shangwe.
Bao la kwanza la Chelsea lilifungwa na Mjerumani Andre Schurrle katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza.
Katika
 mechi nyingine, Real Madrid wamefuzu hatua ya nusu fainali licha ya 
kufungwa mabao 2-0 na Borrusia Dortmund katika dimba la Signal Iduna 
Park.
Madrid wamenusurika kutokana na ushindi wa mabao 3-o walioupata Santiago Bernabeu katika mchezo wa kwanza.
Real wakianza bila ya Cristiano Ronaldo ambaye hakuwa fiti kuanza mchezo wa leo, walikaribia kutolewa na 
vijana wa Jurgen Klopp, lakini jitihada za mlinda mlango wao, Iker Casillas zimewaepushia balaa la kutolewa.
Hata
 hivyo, Real Madrid walikosa penati baada ya winga wake nyota, Angel Di 
Maria kuteleza wakati akipiga tuta hilo, hivyo kipa wa Borussia kuokoa 
kirahisi.
 
Hayajatosha: Marco Reus ameifungia mabao mawili Borussia Dortmund, lakini wametolewa na Real Madrid
 
Bahati
 kubwa: Kipa wa Borussia, Roman Weidenfeller akiokoa penati ya Angel Di 
Maria baada ya nyota huyo raia wa Argentina kuteleza wakati anapiga 
mpira
 
Haamini: Cristiano Ronaldo akiduwaa baada ya Di Maria kukosa tuta
 
Wamekosa bahati: Dortmund walipata nafasi nyingi za kufunga zikiwemo tatu za  Henrikh Mkhitaryan
 

 
No comments:
Post a Comment