Yanga
 imepewa siku 14 kuanzia leo (Septemba 13 mwaka huu) kuwalipa waliokuwa 
wachezaji wake msimu uliopita, nahodha Shadrack Nsajigwa na Stephen 
Mwasika wanaoidai klabu hiyo jumla ya sh. milioni 15.5.
Uamuzi
 huo umefanywa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho 
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana (Septemba 12 mwaka 
huu) ambapo pamoja na mambo mengine ilisikiliza madai ya wachezaji hao.
Fedha
 hizo ni ada ya usajili ambayo klabu hiyo ilikubaliana na wachezaji hao 
wakati ikiwasainisha mikataba. Yanga imeshawalipa sehemu ya fedha 
walizokubaliana na kiasi hicho ndicho bado hakijalipwa. Nsajigwa anadai 
sh. milioni 9 wakati Mwasika ni sh. milioni 6.5.
 


 
No comments:
Post a Comment